HILI ni fumanizi la aina yake! Achana na mafumanizi ya kawaida ambayo yamezoeleka, la safari hii ni la kipekee baada ya mgoni aitwaye Kibole Kalepe kukutwa chumbani na mke wa mtu, Asha Hemedi kisha kukurupuka na kupanda darini haraka kukwepa kipigo.
Tukio
hilo lililofunga umati wa watu wapenda ubuyu lilijiri Oktoba 28, mwaka
huu maeneo ya Iteba-Sinza, jijini Dar baada ya mwenye mali, aitwaye
Fikiri kurejea ghafla nyumbani na kumkuta mkewe akiwa chumbani na Kibole
wakifanya yao.
Mke wa mtu, Asha Hemedi akihamaki baada ya fumanizi.
SIKU YA TUKIO
Kwa
mujibu wa chanzo makini, siku ya tukio Fikiri ambaye ni dereva wa
masafa marefu aliaga kwamba anasafiri lakini akiwa hajafika mbali, gari
liliharibika na kurudi nyumbani kuchukua vifaa na kabla hajagonga
mlango, alisikia sauti ya mkewe na Kibole.
UVUMILIVU WAMSHINDA
Chanzo
hicho kilizidi kushusha mistari kwamba, baada ya kusikia sauti hizo,
Fikiri hakuweza kuvumilia aliamua kuwakatisha kwa kuwagongea mlango huku
akitaja jina la mkewe ili amfungulie lakini hata hivyo ilichukua muda
mrefu mlango kufunguliwa.
MLANGO WAFUNGULIWA
“Mume
aliendelea kugonga mlango, baada ya muda mrefu kupita ukafunguliwa
ambapo mke alikutwa akiwa ameloa jasho na kuhema kwa kasi kutokana na
hofu, hata hivyo alikua amefunga khanga moja tu.
MGONI JUU YA DARI
“Mume
alipoangalia kila kona kumtafuta mwanaume aliyekua naye hakumuona na
alipochungulia darini alimuona mgoni wake amejificha, baadaye aliomba
wapigiwe simu polisi waje kumuokoa,” kilisema chanzo.
ACHIMBWA MKWARA
Chanzo
hicho kilizidi kumwaga ubuyu kwamba, wananchi wapenda mambo ya watu
waliokuwa wamezingira nyumba hiyo walimwambia yeye ni mwizi hivyo
watamshushia kipondo hevi, mgoni huyo alikataa na kudai kwamba hakuwa mwizi bali mgoni hivyo wasimuue.
“Jamani mimi siyo mwizi mimi ni mgoni, niitieni polisi,” alisikika Kibole.
POLISI WAMTAITI
Wananchi
walimuelewa wakaita polisi ambapo ndani ya muda mfupi walifika na
kumshusha darini kisha kumkamata na mwananke wakawapeleka Kituo cha
Polisi Magomeni.
Hakuna maoni: