Header ads

Header ads
CLUB MASAI KAHAMA
» » Makubwa Haya: JAMAA ANASWA AKIPELEKA SIMU GEREZANI ZIKIWA ZIMEFUNIKWA NYAMA

SeeBait

Jeshi la Magereza limefanikiwa kumkatamata Ramadhan Nombo mkazi wa Mabibo jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za kutaka kuingiza simu tano kinyume cha sheria katika gereza la Keko wilayani Temeke.
Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dar es Salaam, Augustine Mboje jana alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 11 jioni katika gereza hilo.
Alisema Nombo anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kuanzia 30 na kuendelea alidakwa wakati akifanyiwa upekuzi katika eneo maalumu la ukaguzi wa wageni mbalimbali wakiwamo wanaowatembelea ndugu na marafiki walioko mahabusu kwenye gereza hilo.
“Huyu (Nombo) alikuwa katika foleni ya mstari wa mwisho ya watu wanaokwenda kuwaaona ndugu zao walioko ndani ya gereza hili. Nadhani hakujua kama sisi kama magereza tuna vifaa vya kisasa vya ukaguzi.
“Ilipofika zamu yake askari wetu walimfanyia ukaguzi na kabla haujaisha kifaa hiki maalumu kiliita alamu kuashiria kuna kitu tofauti,” alisema Mboje.
Alisema alibainika kuwa na simu hizo alizozifunga kitaalaamu na kuficha katika mapande ya nyama yaliyopikwa kwa ustadi wa juu na kuchanganywa na viazi aina ya mbatata.
Mkuu huyo wa magereza, alisema tukio hilo siyo la kwanza katika gereza hilo kwani linatokea katika magereza mbalimbali ya Mkoa wa Dar es Salaam likiwamo la Segerea.
“Wengine wanatumia hadi mbinu ya kuficha simu hizi katika ugali na mikate lakini tunafanikiwa kuwakamata kutokana na uimara wa vifaa na askari wetu,”alisema Mboje

About Unknown

Kwa jina Naitwa MWEUSI waweza wasiliana nami namba 0757420837, 0629208856 au email: timotheosodoka@gmail.com
«
Next
Chapisho Jipya
»
Previous
Taarifa za zamani

Hakuna maoni:

Leave a Reply