Header ads

Header ads
CLUB MASAI KAHAMA
» »Unlabelled » ANAYEDAIWA KUMPA MIMBA MBWA KORTINI


Cecilia Hamis (kulia) akiwa na mume wake (mtuhumiwa) Hamis Juma.

LILE sakata la mume aliyetajwa kwa jina la Hamis Juma (pichani akiwa na mkewe), mkazi  wa Majohe Mji Mpya, Ilala jijini Dar kudaiwa na mkewe, Cecilia Hamis kwamba amempa mimba  mbwa yameibuka mapya, limeyanyaka.

Ijumaa iliyopita, tulifika kwenye ofisi za Taasisi ya Kutetea Haki za Wanyama ambapo mmoja wa maofisa aliyedai si msemaji maalum, alisema wapo katika mchakato wa kufuatilia madai ya mke wa mtuhumiwa huyo kisha kumpandisha mahakamani kujibu mashitaka ya kumdhalilisha mnyama huyo.
“Sisi ishu yetu si kufuatilia kama kweli amempa mimba bali ni kujiridhisha kama kweli yule mzee ametembea na mbwa hilo linatosha kabisa kumfikisha kortini,” alisema afisa huyo na kuomba jina lake lisitajwe.
WAGOMA MBWA KUUAWA
Jingine jipya lililotua linadai kuwa, baadhi ya majirani wa nyumbani kwa Hamis wamegoma mbwa huyo kuuawa baada ya wengine kutaka kufanya hivyo wakisema hali hiyo itaweza kusababisha mdaiwa huyo kufanya matukio mengine nje ya nyumba yake.
MENGINE TENA
Katika hatua nyingine, limebaini kuwa, kumbe mwanaume huyo ana sakata lingine ambapo ana kesi kwenye Mahakama ya Mwanzo Ukonga jijini Dar  akikabiliwa na tuhuma za kumfanyia fujo jirani yake.
Kwa mujibu wa taarifa za kimahakama, ilidaiwa kuwa Hamis alifika nyumbani kwa Alanus Haule ambaye ni jirani yake saa saba usiku wa siku ya tukio akiwa na  silaha za kienyeji na chepe akiwa amelewa na kuanza kumtolea maneno ya vitisho huku akijua ni kosa kisheria chini ya kifungu cha sheria 89 (1) B CAP 16.
Kesi hiyo yenye No 873/2014 ambayo inasikilizwa na Hakimu Mwandamizi, Raia Omary kwa mara ya mwisho ilisikilizwa Julai 3, mwaka huu na kuahirishwa hadi Septemba 11, mwaka huu na yuko nje kwa dhamana.

About Unknown

Kwa jina Naitwa MWEUSI waweza wasiliana nami namba 0757420837, 0629208856 au email: timotheosodoka@gmail.com
«
Next
Chapisho Jipya
»
Previous
Taarifa za zamani

Hakuna maoni:

Leave a Reply