Inasikitisha
sana kifo cha huyu bwana Leonard Mtensa kilichotokea ndani ya gari
lake, mpenzi wake anashikiliwa na polisi kwa uchunguzi zaidi. Hapa chini
ni picha ya huyo dada na picha ya marehemu.
Jackline Hassan mwenye umri wa miaka 25 aliyekuwa na marehemu
Huyu ndiye marehemu bwana Leonard Mtensa alikutwa na mauti ndani ya gari lake aina ya IST akiwa na mwana dada anayefahamika kama jack .
Jeshi
la polisi mkoa wa Kagera linachunguza kifo cha ghafla cha Bw. Leornald
Mtensa Stephen mwenye umri wa miaka 50 ambaye ni mmiliki wa club ya
Lina's night club.
Tukio hilo limetokea mnamo tarehe 18 mwezi huu majira ya saa nne usiku maeneo ya Buyekera manispaa ya Bukoba.
Kwa mujibu wa taarifa ya jeshi la polisi kwa vyombo vya habari ni kwamba
Marehemu alikuwa katika mizunguko na gari lake lenye namba za
usajili T982 CQG aina ya IST na mwana dada Jacline Hassan mwenye umri
wa miaka 25 mkazi wa Buyekera.
Wakati marehemu akiwa na mwana dada huyo ghafla hali yake
ilibadilika na kukimbizwa katika kituo cha afya cha LCT NDOLAGE iliyopo
Manispaa ya Bukoba wakiwa njiani marehemu alifia njiani.
Ndani ya gari lake kulikutwa na Wisky aina ya Bond 7 aliyokuwa anakunywa marehemu.
Mwana dada Jackline Joseph anashikiliwa na jeshi la polisi hadi hapo
uchunguzi utakapokamilika, sababu ya kifo hicho bado haijafahamika.
Hakuna maoni: