Header ads

Header ads
CLUB MASAI KAHAMA
» » RUTO ANUNUA HELIKOPTA YA KISASA YENYE GHARAMA KUBWA


Kwa mujibu wa vyanzo vya kuaminika katika ofisi ya Ruto, amenunua helikopta hiyo aiba ya Airbus H145, huku ikikamilisha taratibu na kwamba itawasili nchini Juni.

Ruto atakuwa mtu binafsi mwenye kumiliki helikopta inayoweza kufanya shughuli zake hata nyakati za usiku. Jeshi la Ulinzi la Kenya (KDF) na polisi ndiyo yenye helikopta zenye uwezo huo.


Kwa mujibu wa jarida la Business Jet Traveler, helikopta hiyo mpya imegharimu Dola 9.7 milioni za Marekani (Sh970 milioni za Kenya).

Inaelezwa kuwa inaweza kutembea kilomita 480 kwa saa na ina uwezo wa kubeba abiria wanane.

Wanasiasa wanaomiliki helikopta

Wanasiasa wakiwamo viongozi wa vyama, magavana, maseneta, wabunge na wanaelezwa kuhitaji helikopta za kisasa.

Katika miaka miwili iliyopita, Rais Uhuru Kenya, Kiongozi mkuu wa upinzani, Raila Odinga, Kalonzo Musyoka, Musalia Mudavadi na Peter Kenneth walielezwa kuwa waliomba kununua helikopta.

About Unknown

Kwa jina Naitwa MWEUSI waweza wasiliana nami namba 0757420837, 0629208856 au email: timotheosodoka@gmail.com
«
Next
Chapisho Jipya
»
Previous
Taarifa za zamani

Hakuna maoni:

Leave a Reply