Header ads

Header ads
CLUB MASAI KAHAMA
» » Muimbaji wa wimbo ‘Lambada’ Loalwa Braz wa Brazil afariki dunia

Muimbaji wa Brazil, Loalwa Braz, aliyejipatia umaarufu kwa wimbo wake wa mwaka 1989 ‘Lambada’, amekutwa amefariki kwenye gari iliyoungua moto mjini Rio de Janeiro.
Loalwa Braz akiwa na Akon backstage mwaka 2012 kwenye tuzo za Billboard Latin Music Awards, Miami, Florida
Mwili wa muimbaji huyo aliyekuwa na miaka 63 ulikutwa karibu na nyumbani kwake huko – Saquarema.
Polisi bado hawajaweza kutambua sababu ya kifo chake.
Braz alikuwa muimbaji mkuu wa kundi Kaoma lililokuwa na makazi Ufaransa na Brazil na , lililopata umaarufu kwa wimbo Lambada. Msanii wa Marekani, Jennifer Lopez aliwahi kusample wimbo huo kwenye hit yake ya mwaka 2010, On The Floor

About Unknown

Kwa jina Naitwa MWEUSI waweza wasiliana nami namba 0757420837, 0629208856 au email: timotheosodoka@gmail.com
«
Next
Chapisho Jipya
»
Previous
Taarifa za zamani

Hakuna maoni:

Leave a Reply