Header ads

Header ads
CLUB MASAI KAHAMA
» »Unlabelled » MAMA TIBAIJUKA ANUSURIKA KIFO BAADA YA GARI LAKE KUGONGA PUNDA WILAYANI KAHAMA


Waziri wa  ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Profesa Anna Tibaijuka amenusurika kifo baada ya gari alilokuwa akisafiria kutoka Wilayani Muleba kwenda Dodoma kugonga  punda katika kijiji cha Wendele Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga
 
  Mashuhuda wa tukio hilo walisema lilitokea jana majira ya saa 11  jioni ambapo gari lenye namba za usajili STK 5857mali ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya makazi lililokuwa likiendeshwa na dereva Linusi Eliasi (42) liligonga  punda aliyekatiza ghafla barabarani.
 
Akielezea zaidi kuhusu ajali hiyo kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga Kihenya Kihenya amesema  Waziri Tibaijuka alikuwa na baadhi ya wanafamilia wake katika gari hilo wakitoka Muleba kwenda Dodoma kwa ajili ya kuwahi shughuli za Bunge zinazoendelea ,Hata hivyo hakuna alie jeruhiwa nampaka sasa waziri yupo vizuri.
  GARI YA WAZIRI TIBAIJUKA

About Unknown

Kwa jina Naitwa MWEUSI waweza wasiliana nami namba 0757420837, 0629208856 au email: timotheosodoka@gmail.com
«
Next
Chapisho Jipya
»
Previous
Taarifa za zamani

Hakuna maoni:

Leave a Reply